LIKE UKURASA HUU KWA HABARI ZAIDI

Powered By Blogger Widgets


.

Thursday, October 6, 2016

Kidoa Adai 'Anayenitaka Anifuate na Mabunda Yakutosha'

0 comments

Staa anayepamba video za wasanii mbalimbali wa Bongo Fleva a.k.a Video Queen, Asha Salum ‘Kidoa’ amefunguka kuwa malipo kidogo anayopata kutokana na kazi hiyo yamemfanya aamue kukaa pembeni na kugeukia uigizaji.

Akizungumza na Gumzo la Town la Mtanzania
Jumamosi, Kidoa amesema kwa sasa yupo bize zaidi katika uigizaji wa tamthilia na filamu mbalimbali.

Anasema: “Hakuna kitu kwenye u-Video Vixen, tunalipwa kidogo sana. Kwa sasa sitaki tena. Naweza kusema hakuna cha maana zaidi ya kuonekana… lakini kama mtu akija na pesa ya maana, naweza kushiriki kwenye video yake.”

Alipoulizwa pesa ya maana ni kiwango gani, haraka alisema: “Pesa ya kueleweka. Nimechoka kufanya kazi isiyokuwa na malengo, mtu akija na milioni yake, naingia mzigoni. Chini ya milioni moja, sishiriki video ya msanii kabisa.”

“Niseme ukweli, kwa sasa najivunia nimekuwa hot cake kwenye tamthilia… natafutwa sana na ninafanya kazi hata tano ilimradi tukubaliane.

“Ujue tamthilia na filamu wananilipa vizuri sana, pesa ambayo sijawahi kulipwa na ninahisi huko kwenye video za wasanii sikuwahi kufikiria kupata fedha kama hizi, ndiyo maana nimefumbuka macho na kuitambua thamani yangu,” anasema.

Anasema pamoja na kwamba kwa sasa amepata
mapokezi mazuri na makubwa kwenye tamthilia na filamu, awali walimgomea wakidhani hana kipaji.

“Mimi kipaji changu hasa ni uigizaji, sikuwa na ndoto za kuwa Video Vixen kabisa. Niliwafuata baadhi ya wasanii na watayarishaji wakubwa lakini walinitosha wakiamini labda sina kipaji, lakini leo hii wameona uwezo wangu wamenikubali.

“Siwezi kukataa kuwa video za wasanii wa
Bongo Fleva zimenisaidia, kwakweli zimenitoa lakini hazilipi. Maisha siyo kuonekana tu, lazima uwe na kitu unaingiza ndiyo utaona raha ya kazi,” anasema Kidoa ambaye video ya Akadumba ya msanii Ney wa Mitego ndiyo iliyomtambulisha.

-Mtanzania
Read More ->>

Wimbo wa Chura Kutoka Kwa Snura Sasa Ruksa Kupigwa Maredioni na Kwenye TV.

0 comments

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye amemruhusu msanii wa muziki, Snura Anthony Mushi ‘Snura’ kuachia video yake mpya ya wimbo ‘Chura’ baada ya msanii huyo kufanya marekebisho ya video ya wimbo huo na kukubaliwa na wizara.

Aidha, katika barua ya wizara imemtaka Snura kuomba radhi mbele ya waandishi wa habari ili video hiyo ianze kuchezwa. Mapema mwaka huu video ya wimbo huo ulitangazwa kufungiwa na serikali baada ya video hiyo kukosa maadili ya kitanzania.

Akiongea na waandishi wa habari katika ukumbi wa Maisha Basement jijini Dar es salaam, Snura amesema anamshukuru Mh waziri Nape Moses Nnauye kwa kumkubalia ombi lake la kuiruhusu kazi hiyo kutoka.

“Mh Nape ameuruhusu wimbo wangu mpya wa Chura na video Chura kupigwa na kuonyeshwa katika vituo mbali mbali vya radio na runinga baada ya kuona video yangu mpya ya wimbo ina maadili na ujumbe ndani yake ikiwa ni kukidhi makubaliano ya awali kwamba wimbo wangu ‘Chura’ utafunguliwa pale nitakapofanya video mpya ya muziki yenye maadili ya kitanzania,” alisema Snura.

Aliongeza, “Video yangu mpya Chura inaeleza maana halisi ya neno Chura. Chura ninayemzungumzia ni mwanamke anayeruka ruka katika mahusiano kwa kubadilisha wanaume mbalimbali matokeo yake kupata magonjwa sugu,”.

Pia katika barua hiyo ya Mh Waziri wa habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye amempa onyo kali msanii huyo kutokurudia kufanya tena video zisiyokuwa na maadili ya kitanzania.

Read More ->>

VIDEO: Utani wa Mchekeshaji Eric Omondi Kwa Wanaotaka Kuwa Kama Rais Magufuli.

0 comments
Eric Omondi raia wa Kenya ambaye ni moja kati ya watu waliobarikiwa vipaji vingi ikiwemo uwezo binafsi wa kuchekesha kupitia maneno na mwili wake pia.

Baada ya kufanya ile ya mambo ya kuzingatia kwa wale wanaotaka kuwa kama Diamond Platnumz, Akothee, leo katusogezea nyingine ambayo inamhusu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Magufuli. Eric Omondi katuletea mambo muhimu unapaswa kuyazingatia kama unatamani kuwa kama Rais Magufuli

Unaweza kumtazama Omondi kwenye hii video hapa chini…

Read More ->>

BSS Kuna Uchawi Gani? Mbona Wengi Hawafanikiwi?

0 comments

Waungwana leo kwenye pita pita yangu nilikutana na miongoni mwa washiriki wa BSS aliyekuwa miongoni mwa waliofanya vizuri (jina kapuni) akiwa kachoka sana mpaka nikamuonea huruma, sasa nikawa najiuliza hivi hili shindano lina manufaa gani? Kwa nini washiriki wengi hawafanikiwi na majina yao hufifia baada ya muda mfupi?

Tuchukulie mfano mtu kama Jumanne Idd mpaka leo hajulikani halipo alkadharika Walter Chilambo, Kayumba , AngelMarry Kato , Steven Lupenza, Nasibu Fonabo nk ni miongoni mwa vijana ambao wana uwezo mkubwa sana wa kuimba lakini cha ajabu hawafanikiwi kulinganisha na washiriki wengine kama vile Harmonize ingawa alitoka mapema na kuonekana si chochote leo hii katudhihirishia kwamba yeye ana uwezo gani....

By Hance mtanashati
Jibu la Mdau
Kwanza ni jambo la kujiridhisha kuwa si BSS tuu bali hata huko nje shows kama za the voice, SA idols, xfactors, na Got talents za nchi nyingi, ni watu wachache sana walio shinda mashindano ya aina hii wame make ki muzik.
Kwanini!!?
1. Lengo la mashindano, waandaji huwa wanaandaa kwa ajili ya faida yao na kupata wadhamini, na mara nyingi wakisha maliza shindano hawawekezi kwa nguvu kubwa kwani kuna shindano la mwakani inabidi waandae tena, hawana time na wewe
Pia washindanaji lengo lao kubwa zaidi ni kupata yale mamilioni tuu, wakisha pewa kuna msemo unasema easy come easy go
2. Mashabiki wa mashindano, askudanganye mtu, watanzania wanao fuatilia BSS ni chini ya milioni 10, wanao piga kura ni chini ya laki moja, kwa hiyo kama msanii ukishinda unakuwa hujapata fan base kubwa bado isipo kuwa ki portion kidooogoo cha wale walio angalia na wakajisumbua hata kupiga kura,,na wengi wanai piga kura huwa wanaanza kwanza kukuonea huruma ya kimaisha mfano unakumbuka Jumaanne Idd kwa hiyo Raymond akitoa wimbo mmoja uka hit anapata fan base kubwa kuliko wewe mshindi
3. Mziki ni zaidi ya kukopi nyimbo za watu, angalia yule mshindi wa mwaka jana kayumba alishnda kwa kuimba imba taarab za kina isha mashauz sasa je akitoka BSS ana uweza huo mziki!!? Mpaka yeye mwenyewe hajui afanyeje yaani
*Sababu ni nyingi lakini kikubwa ni wasanii wajiamini wahue uwezo wao ni zaid ya kuimba BSS, ndio maana mara nyingi unakuta wanao fanikiwa ndio wale walio shika u tano, au ukumi, kwa kuwa it takes more than to win BSS ili kuwa msanii
By Ice Man 3D

Read More ->>

Jinsi ya Kumtuliza Mumeo Asitoke Weekend.

0 comments


Siku hizi wa naume licha ya kukimbia nyumba zao kwa kisingizio cha kazi maajabu weekend hasa Jumamosi utasikia wanaaga nafika hapo njiani naja naenda kununua gazeti.

Kumbe wanaenda kunywa supu na mambo mengine unasubiri wee mpaka alasiri au jioni

Hivyo wanandoa wengi hili limekuwa tatizo mwanaume kiguu na njia asb mchana na njia kumuacha mama na watoto.

Nini kifanyike hasa weekenda Mwanaume ashinde NYUMBANI akikupumzikia??

Zipo njia nyingi mojawapo SUPU YA WEEKEND NA MAZUNGUMZO NA MKAO

Ni kweli wanawake wengi hamjuagi kuwakalisha waume home.

Anza hivi
Siku uko home wewe amka mapema kabla yake anza makeke jikoni…

Mara blenda priiiii… juice… ama milk shake…. hahahaha..Utaona anasogea jikoni..

Wakati anakunywa juice ama milk shake…Anza kukuna nazi…

Chambua mnafu…

Hapo jikoni kuna kanyama kanachemka… katia kitunguu tupia viazi 2 na ndizi.Hahaha..

ile harufu ikianza kutoka utasikia anafuata maji jikoni… hahahaha kwenye friji… wala hatumi..

Hahaahha… utasikia nini kiko jikoni?Hahahaa.

Mmiminie supu…

Na ndizi mbili na kiazi kimoja kapilipili mbuzi pembeni..

Muulize kuna chapati…Mpe.. hahahahaha..Akimaliza supu nakuapia atasinzia..

.Akishtuka ugali na mnafu na nyama umeiva…Mpe ale..Mshushie na glass ya mtindi…Hahahaha..

analewa full Hata kama kuna mama junior anaambiwa usipige…

Hahahahahaha….Baada ya hapo acha apumzike… aoge…

Kisha funga ka khanga kako kepesi jilaze pembeni.. woiiiiiiiii..


Mkimaliza muombe pesa ya sokoni…

NAKUAPIA HATA KAMA JANA YAKE ALIKUPA ATAKUPA TENA.

Hahahahaha.. jamani…

Hahahahaha… yani kwa raha ya supu… nakuapia utaambiwa hata mama alipiga simu jana… hahahaha.. ama utasikia mamii.. njoo uone njoo… unaitiwa kitu cha kwenye tv.. hahaha.

Hata hujaona mwanzo ila kwa raha yakasupu utaitwa…

Hata kama huna kalio nakuambia utapigwa kibao hata cha mgongo…. hahahahahahahahahaha.

Sasa wewe unaamka chai na mkate kama chuo cha uhazili…
Wali maharage kama jeshi...


Read More ->>

Diamond Afunguka Haya Kuhusu Issue ya Mama yake Kutopost Picha ya Zari Siku ya Kuzaliwa Kwake.

0 comments


Habari za kuwepo kwa bifu kati ya Mama mzazi wa Nassib Abduli aka Diamond Platnumz na Zari ambayeni mpenzi wa msanii huyo na Mama wa mtoto wake wa kwanza zilichukua sura mpya.

Mwezi uliopita baada ya Mama mzazi huyo kutopost picha ya Zari kwenye BirthDay yake na kuja kupost picha ya Wema Sepetu akimtakia Birth Day njema.

Kwenye The Playlist ya Times FM, Diamond aliulizwa swali hilo ambapo alifunguka kwa kusema kuwa inabidi ifike mahala kuwa wawape watu kitu cha kuzungumza kwakuwa kibongo bongo familia yao inatizamwa kama ya kina Kardashian.

“Sisi ndio pambo la mitandao, Mtu akiamka lazima aingie kwenye familia ya kina Diamond ajue inafanya nini, ni familia ambayo ina mshikamano na ipo kibiashara zaidi”.
“Inabidi tuwape watu vitu vya kuzungumza zaidi, Kila kinachofanyika kinafanyika kwa makusudi na Mama yangu na Zari wanaelewana sana, ndio maana Zari yupo Tanzania kwa sasa”


Read More ->>

Hii ndo Sababu Inayomfanya Mwanamuziki Diamond Asishiriki Fiesta 2016.

0 comments

Hatimaye Diamond ametoa sababu ya kutopanda jukwaa la fiesta 2016,Akihojiwa na kipindi cha jahazi cha clouds fm Diamond amesema kuwa ndoa (mkataba) yake na Kampuni ya Simu ya Vodacom ndio sababu inayomfanya asishiriki Fiesta mwaka huu...
Wadhamini wakuu wa Fiesta ni Tigo hivyo kufanya hivyo kungeleta mgongano wa maslahii....

Read More ->>

HUYU NDIO SCORPIONI MTOBOA MACHO WA BUGURUNI AKIWA MAHAKAMANI

0 comments





 

Pichani : Scorpion, mwenye fulana nyekundu, akiwa mahakamani leo chini ya ulinzi mkali wa polisi.
Leo katika mahakama ya wilaya ya Ilala, mkazi wa buguruni kwa mnyamani anayetuhumiwa kuwachoma watu visu na kisha kuwatoboa macho, Salum Henjewele maarufu kama Scorpion amepandishwa kizimbani na kusomewa tena shtaka la unyang’anyi wa kutumia silaha .
Kesi ya Scorpion, ambaye alikamatwa baada ya kumchoma visu na kisha kumtoboa macho, Said Ally mkazi wa mabibo Hostel, inasikilizwa na hakimu Adolf Sachore.Leo kesi hiyo ilipangwa kwa ajili ya kutajwa na upande wa mashtaka umeieleza mahakama kuwa upepelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na hivyo mtuhumiwa amerudishwa rumande


Read More ->>

Sunday, July 12, 2015

MH MAGUFULI NA JANUARY WAANGUA KICHEKO CHA FURAHA.......!!

0 comments



Read More ->>

KIGOGO WA WEMA KORTINI.

0 comments
Jamaa aliyewahi kudaiwa kuwa karibu na mwigizaji Wema Sepetu anayejulikana kwa jina la Clement Mwankayi Kiondo ‘CK’ au Kigogo wa Wema na mwenzake, Emmanuel Kagondela wamepandishwa kortini kwa mashitaka mawili ya kughushi hundi kisha kuchota fedha.
Clement Mwankayi Kiondo ‘CK’ akiwa chini ya ulinzi mkali wa polisi.
Wawili hao walipandishwa kizimbani juzi (Alhamisi) katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar.
Katika kosa la kwanza, CK alidaiwa kutenda kosa la kughushi hundi no 302002 yenye thamani ya zaidi ya Sh. milioni 100 kutoka kwenye Ofisi ya Waziri Mkuu huku akijua kuwa ni kosa kisheria.
Katika kosa la pili, CK ambaye aliwahi kudaiwa kumgombanisha Wema na Kajala Masanja kwa pamoja na Emmanuel, mnamo Machi 13, 2014 walikula njama za kuiba kiasi cha Sh. milioni 100 katika Benki ya NBC, Tawi la Ilala jijini Dar.
Kesi hiyo ambayo ilisikilizwa mbele ya Hakimu Huruma Shahid na Wakili wa Serikali, Aloyce Mbumito, ilidaiwa  mnamo Machi, 2014 kwa nyakati tofauti, jamaa hao walitumiwa kughushi hundi kwenye ofisi hiyo ya Waziri Mkuu.
Katika kujibu tuhuma hizo, washitakiwa wote kwa pamoja  walikana mashitaka na kesi hiyo iliahirishwa hadi Julai 23, mwaka huu.
Katika kesi hiyo watuhumiwa hao walipaswa kuwa na wadhamini wawili-wawili wanaotambulika na kiasi cha Sh. milioni 10 kila mmoja kwa ajili ya kupatiwa dhamana.

Read More ->>

MAGUFULI NDIYE MGOMBEA URAIS WA CCM 2015.....!!!

0 comments
magufuli
MBUNGE wa Biharamulo Mashariki (CCM) na Waziri wa Ujenzi, Mhe. John Pombe Magufuli ameshinda katika uchaguzi wa kumpata mgombea urais wa CCM kwa mwaka 2015. Magufuli ameshinda baada ya kupata jumla ya kura 2104 sawa na 87.1%, Balozi Amina Salum Ali amepata kura 253 sawa na 10.5% na Dk. Asha-Rose Migiro 59 sawa na 2.4%.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Anne Makinda ndiye aliyepewa jukumu la kusoma mshindi katika kura za Kikao cha Mkutano Mkuu wa CCM kilichofanyika kuanzia jana na kuendelea leo asubuhi mkoani Dodoma.
KURA ZILIZOPIGWA: 2422
KURA ZILIZOHARIBIKA: 6
KURA HALALI: 2416


Read More ->>

Meet Catherine Magige the hottest MP from Arusha....Just see how S3xy she is...Photos

0 comments



Read More ->>

Hatua 4 Alizopitia Magufuli Kushinda CCM. Huwezi Kupenya Bila Kuzivuka Hizi. Zisome Hapa

0 comments
Read More ->>

MEEK MILL AKANA KUMUIBA NICKI MINAJ......!!!!

0 comments
 
 Rapa Meek Mill.
New York Marekani
RAPA Meek Mill ameamua kufunguka kuwa hakumuiba mpenzi wake wa sasa, Nicki Minaj kutoka kwa mpenzi wake wa zamani, Safaree Samuels ambaye alidumu na Minaj kwa miaka 12.
 
Rapa Meek Mill akiwa na mpenzi wake Nick Minaj.
“Awali, sikuwa na mipango na Nick kabisa, uhusiano wetu umetokea tu na wala sihusiki katika kuvunjika kwa penzi lake na mpenzi wake wa zamani,” alisema Meek.
Read More ->>

Yule Muhindi Aliyekamatwa Dodoma Na Mabilioni Ya Hela Ya Kuwahonga Nec, Aelezeaa Kila Kitu, Na Zile Pesa Zilikuwa Zinatoka Kwa Mfanya Biashara Mkubwaa....

0 comments

Read More ->>

ZITTO KABWE ADHIHIRISHA NI TIMU EDWARD LOWASA..........!!

0 comments
Chama cha ACT Wazalendo kimekuwa kikidaiwa kufadhiliwa na mwanasiasa mgombea urais Edward Ngoyai Lowasa.Hii ni moja ya kithibitisho uhusiano wa kiongozi mkuu wa chama hicho na waziri huyo mstaafu.
Read More ->>
 

The Best new logo

ADVERTISE HERE

NDEGE TAUSI

| THE BEST © 2013. All Rights Reserved | Template Style by The Best | Design and coded by 0754893991 | Back To Top |