LIKE UKURASA HUU KWA HABARI ZAIDI

Powered By Blogger Widgets


.

Sunday, July 12, 2015

MAGUFULI NDIYE MGOMBEA URAIS WA CCM 2015.....!!!


magufuli
MBUNGE wa Biharamulo Mashariki (CCM) na Waziri wa Ujenzi, Mhe. John Pombe Magufuli ameshinda katika uchaguzi wa kumpata mgombea urais wa CCM kwa mwaka 2015. Magufuli ameshinda baada ya kupata jumla ya kura 2104 sawa na 87.1%, Balozi Amina Salum Ali amepata kura 253 sawa na 10.5% na Dk. Asha-Rose Migiro 59 sawa na 2.4%.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Anne Makinda ndiye aliyepewa jukumu la kusoma mshindi katika kura za Kikao cha Mkutano Mkuu wa CCM kilichofanyika kuanzia jana na kuendelea leo asubuhi mkoani Dodoma.
KURA ZILIZOPIGWA: 2422
KURA ZILIZOHARIBIKA: 6
KURA HALALI: 2416



SHARE HII HABARI NA RAFIKI ZAKO:
Technorati Digg This Stumble Stumble Facebook Twitter
UPDATE YOUR DAY FOR THE BEST NEWS.

0 comments:

Post a Comment

 

The Best new logo

ADVERTISE HERE

NDEGE TAUSI

| THE BEST © 2013. All Rights Reserved | Template Style by The Best | Design and coded by 0754893991 | Back To Top |